NITAWEZAJE KUISHINDA ZINAA ?~Sehemu ya mwisho.
- Mch. Gasper Madumla
- Aug 13, 2015
- 2 min read

” Ikimbieni zinaa.” 1 Wakorintho 6:18. Na Mchungaji Gasper Madumla.
Bwana Yesu asifiwe…
Njia ya pili ambayo itakuwezesha kuishinda zinaa ni;
▪ Kujitengamanisha na roho ya zinaa.
~Wapo watu ambao wamefungamanishwa na roho za zinaa pasipo kujijua,wanajikuta wakiwaka tamaa katika miili yao. Mfano shetani anaweza akawa amekutafuta katika kila kona ya maisha yako akuangushe,akiona amekushindwa anajaribu akuletee zinaa,hapo sasa anakuja binti/kijana mwenye vishawishi vya hali ya juu akikuanzia mbaliiii kiasi kwamba huwezi kumshtukia kwa haraka na anajua ya kwamba ukidondoka katika dhambi hii si rahisi kuinuka mara moja ikiwa hujadhamilia kikamilifu kwa sababu ya uwepo wa agano la zinaa.
Watu wengi wanazini na kufanya uasherati si kana kwamba wana penda,wengine ni miroho michafu ya zinaa inawasukuma kufanya. Mfano unaweza kukuta binti alinayedondoka dhambini mara kadha wa kadha na ukimuuliza anakujibu ya kwamba hata yeye mwenyewe hajui kwa nini amezini na mtu huyo.
Hili ni tatizo kwa watu wengi,kukumbwa na roho za zinaa. Kanisa la leo nalo limevamiwa na roho ya zinaa,baadhi ya watumishi wamedondokea huko. Dawa ni kujitengamanisha mbali na roho za zinaa,kwanza kwa kuchukia dhambi hii. Kisha kumsihi Roho mtakatifu achukue nafasi ya kuziondoa roho hizi,katika maombi rasmi kabisa ya kuvunja nira ya roho ya zinaa.
▪Kukaa uweponi mwa Bwana.
~ kukaa uweponi ni hali endelevu ya kudumu katika fundisho muda wote hata kama ukiwa unafanya kazi zako binafsi lakini muda wako mwingi una mawasiliano na Mungu. Ni hali ya kushughurika na mambo ya Mungu katik kiwango cha juu. Mtu yeyote mwenye ushirika na Bwana Mungu ni mtu aliyekaa uweponi.
Mfano mdogo ni huu; kama vile bawabu ilivyoungamanishwa na mlango wa chumba. Kiasi kwamba ukiingia chumbani yenyewe unaikuta pale pale,na hata kama ukitoka bado unaikuta pale pale imengangana katika mlango wa chumba,ndio maana Daudi akasema;
” Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu. ” Zab.84:10
Sasa,ukiweza kujibidiisha kukaa uweponi mwa Mungu kama bawabu ilivyoshikamanishwa na mlango,ndivyo mawazo ya zinaa hukosa nafasi na ndivyo hata roho za zinaa hukosa mlango w kukuvamia. Siku zote roho chafu hukaa mahali pachafu,ikiwa hema ya moyo wako ni safi basi ni dhahili kabisa hakutakuwa na zinaa yoyote ile itakayotajwa kwako.
Shida kubwa ni kwamba watu wengi wapo uvugu uvugu katika imani zao,kwa hali ya kuwa uvugu uvugu kwamba unaamini lakini huku bado unaonja onja dhambi hapo ndipo zinaa nayo inakungangania. Bali dawa ya yote hayo ni kukaa uweponi full time.
Ikiwa roho ya zinaa imekukamata kiasi kwamba umejaribu kukimbia lakini hukufanikiwa,tafadhali nipigie basi ili tuombe pamoja ili Bwana akuhudumie.
Kwa huduma ya maombi nipigie sasa kwa namba +255 683 877 900.
What’s app number ni +255 746 446 446
UBARIKIWE.
Comentários