top of page

MATENDO YA HURUMA.

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi… 

Tunaposema “ matendo ya huruma” tunamaana pana kidogo, kwa maana neno “ huruma” ni moja kati ya tabia ya Mungu ( Yoeli 2:13).  Yeye Bwana Mungu amejawa na huruma, ni Yeye aliyekuhurumia wewe,hata leo upo hai unaishi,ni kwa huruma za Bwana tu,kwamba hatuangamii ( Maombolezo 3:22). Hii ina maana kama Mungu singelikuwa wa Huruma,tungelikuwa tumeangamia muda mrefu sana.

Matendo ya huruma yanaweza kuhusishwa na “kuomba kwa wahitaji,kufunga na kuomba kwa wahitaji,kuwapa mahitaji muhimu kama vile nguo,pesa,chakula,malazi,n.k,“. Lakini tendo kubwa la huruma halipo katika mambo hayo yote ambayo wengi hufanya,maana katika hayo hata mataifa hufanya. Bali tendo la huruma ni “ Kuirejeza roho za waliopotea kwa Bwana / to point the lost to Christ”

Fikiria  pale Bwana alipoupenda ulimwengu kiasi cha kuhurumia,Je aliwapa chakula,? Au nguo za kuvaa? Bali alimtoa mwanaye wa pekee. Lengo kuu lilikuwa aliyepotea arejee kwa Bwana. Yamkini kulikuwa na matajiri lakini bado Bwana aliwahurumia. Hakuna huruma kubwa kama hiyo. Hivyo tendo la kwanza na lenye nguvu liitwalo tendo la huruma ni ;

kuhurumia roho ya mtu isipotee,sio mwili wake” .  Bahati mbaya sana,watu wengi hufikiria mambo ya mwili na kuyaacha mambo ya rohoni na ndio maana tunaona leo watu wakibeba sabuni,nguo,chakula kupeleka kwa wahitaji kama matendo ya huruma na wakisha wapelekea basi huondoka. Sasa,roho zao zitaokolewaje ikiwa kama mtazamo wa matendo ya huruma yamefungiwa katika eneo moja tu. Si vibaya hata kidogo kuwasaidia wahitaji,kwa maana hayo ni matendo ya huruma pia,lakini kwanza roho zao ndio muhimu.

Ebu fikiria kama kila mtu angelikuwa anafikiria kuwaendea wahitaji na kuzilisha roho zao,kuzivalisha roho,kuziosha roho zao n.k !!! Hivi ingelikuwaje uzuri wake? Hivi hujui ya kwamba wengine unaowapelekea vitu,ni watu waliofungwa na shetani,shetani kawatia kwenye ugonjwa na wanahitaji msaada wa kiroho kama sehemu ya matendo ya huruma. Lakini cha ajabu unakwenda na bonge la mche wa “sabuni ya mbuni” Kha! Jamani,sasa sabuni ya kuogea itamfunguaje? Unanielewa lakini???

Wahitaji wanahitaji kwanza Neno,sio sabuni zako au nguo zako. Neno litawatoa mahali wapofungwa pamoja na maombi yako. Kisha mkononi wape ulichonacho,la kama huna basi wape Yesu uliyenaye,yatosha kabisa kuwa na mtaji mzuri wa namna hiyo. Ifike wakati tunaposhughulika na matendo ya huruma tufikirie kwanza roho zao, kama Kristo anavyofikira haswa roho zetu.

Wapo wahitaji ambao ukiwapa Yesu,utakuwa umewapa mtaji mkubwa sana kuliko kipande cha sabuni. Lakini pia kumbuka hili; ikiwa unakwenda kumsaidia mtu,huitaji upewe sifa wewe. Bali fanya kama kwa Bwana,tena ikiwezekana usiwapige pich na kuweka kwenye mitandao ili uonekane ukiwasaidia. Ukifanya hivi,utakuwa unajaribu kujisifia wewe,kujionesha kwamba ni wewe ufanyaye hayo,badala ya kumpa Mungu utukufu. Fanya kama kwa Bwana kimya kimya! Na Bwana aonaye sirini atakujaza tu. Kumbuka,sifa na utukufu ni mali ya Bwana.

Ukifanikiwa kujaliwa kuwa na mali au fedha na wewe si mtumishi uwezaye kufasiri Neno la Mungu. Basi chukua watumishi wawili watatu watakao sema habari za huruma ya Yesu kwa usahihi kwa wahitaji hao. Na wewe utoe kile ulichonacho ili kusudi kwa pamoja muwe mmefanya kazi ya Bwana kwa kushirikiana.

Kwa msaada zaidi,pamoja na maombi piga kwa +255 683 877 900

Whatsapp namba +255 746 446 446

Mch. G. Madumla.

UBARIKIWE.

Comments


Post: MAFUNDISHO

Follow

  • Facebook
  • Twitter

©2022 by MAFUNDISHO YA NENO LA MUNGU. Proudly created with Wix.com

bottom of page